HII NI WEB YA KIDINI
2 comments on HABARI
Add a comment
To add comments without entering your email and image verification, you must be logged in. Login or Join Blogster
On 3 months ago
HII NI WEB YA KIDINI
To add comments without entering your email and image verification, you must be logged in. Login or Join Blogster
To email posts to friends, you must be logged in. Login or Join Blogster
www.allymadulu currently has no Blogster friends
Add her as a friend and send her a friendly welcome!
Enyi waja wa mwenyezi mungu ninakuusieni na kuiyusia nafsi yangu kumcha mwenyezi mungu (s,w) kwa kutekeleza ibada ya zakati, ni pale aliposema Allah (sw) chukua katika mali zao sadaka (Dhaka) uwatohalishe na kuwatakasa…
ndugu waislam hakika jambo la zakaati katika uislam ni jambo kubwa! nalo ni moja kati ya nguzo za uislam ambalo limeambatana na ibada ya salah, katika sehemu nyingi katika aya za Qur`aani tukufu,Na alikuwa mtume (saw) akihimiza kwa mahimizo makubwa kwa kuwatuma masahaba kwenda kwa matajiri na wanaohusika ili kuchukuwa Dhaka na kuwagawia wanaohusika kupewa Dhaka hiyo, Na jambo hilo la Dhaka wakaliendeleza masahaba waongofu,na kwa ukubwa wa jambo hilo masahaba walihesabu kuwa ni ukafiri kwa waislam waliozuia kutoa Dhaka na waliwaandalia majeshi iwe tayari kwa kuwapiga vita na kuwaua kama alivyofanya miongoni mwa masahaba wakubwa seyyidina Abubakari saddiq (r,a)kwa kuwaandalia jeshi baadhi ya waislam ambao waliasi kutoa dhaka katika utawala wake, ila pale walipotii aliwasamehe na kuaza kukusanya Dhaka.
Enyi ndugu waislam yeyote mwenye kukataa kutoa Dhaka katika mali yake basi huyo ni kafiri alieritadi kwa kutoka katika uislam na analazimika kutubia! Na kama hakutubu kwa kutekeleza ibada hiyo basi uhuwawa kwa sababu amekadhibisha aya ya mwenyezi mungu mtukufu na mtume wake (s,a,w) na kwa ijmaai (makubaliano) ya viongozi wa kiislam ambao wao ni warithi wa mitume.
Enyi ndugu waislam hakika makemeo ya kuacha kutoa Dhaka ni makubwa mno na yanapelekea adhabu hapa duniani na kesho akhera kama mwenyezi mungu alivyobainisha katika maneno yake kuwa:wala usiwadhanie wale wafanyao ubakhiri katika yale aliyowapa mwenyezi mungu katika fadhira zake kuwa ni bora kwao! Laa bali hiyo ni shari kwao, watafungwa makongwa kwa yale waliyokiyafanyia ubakhiri…(3:180).Kwa hiyo ndugu waumini huo ni uovu mkubwa na shari mbaya sana kama waislam hatutahimizana kutekeleza ibada ya dhakaati na tufahamu ya kuwa tunatangaza vita na mwenyezi mungu kwa kupuuza ibada hiyo.Je ndugu wailam tutaweza kupigana vita na mwenyezi mungu?Na akasema tena kwa wale waliolimbikiza fedha na dhahabu na wala hawatoi katika njia ya mwenywzi mungu kuwa wape habari ya adhabu iyumizayo siku ambayo(mali zao ) zitakapotiwa moto katika moto wa jahannamu, na kwayo vita chomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao,(na isemwe)haya ndio mliyolimbikiza kwa ajili ya nafsi zenu,basi onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa mnalimbikiza (9:34-35).Ninakuhusieni pamoja na kuiyusia nafsi yangu kwa kauli ya mtume (s,a,w) Aliyosema kuuwambia umma wake kuwa pindi watu wakijilimbikizia dhahabu na fedha kwa kuto kutoa Dhaka na sadaka basi muumini wewe rimbikiza maneno haya (katika moyo wako kwa kuomba dua ) Ewe mwenyezi mungu hakika mimi ninakuomba uthibiti katika amri (zako), na azma (nia) juu ya uongofu, na ninakuomba kushukuru neema zako, na ninakuomba (niwe na ) moyo uliosalimika na (madhambi), na ninakuomba ulimi wenye kusema kweli, na ninakuomba miongoni mwa kheri zozote unazozijuwa, na ninakuomba msamaha kwa unayoyajuwa! Hakika wewe ni mjuzi mno wa mambo ya siri
wewe nani